Jinsi ya kukabiliana na makwazo ya awali ya mwanamke
KWA mtu ambaye ndiyo kwanza anajiingiza katika ulimwengu wa mapenzi, ni dhahiri kuwa atakutana na mambo mengi ya kumkwaza, ambayo hatimaye yanaweza kumvunja moyo kuhusiana na suala zima la mapenzi. Wanaume, hususan kwa kuwa ndio wenye jukumu la kuanzisha mahusiano, hujikuta katika wakati mgumu wanapokwenda kukabiliana na wanawake, kutokana na tabia za wanawake, hasa wasichana za kutaka kujilinda.
Wanaume wengi wamekata tamaa na kubaki wakinung'unika, kutokana na kusalimu amri kwa makwazo mbalimbali yatokanayo na tabia ya asili ya mwanamke, ya kumjaribu mwanaume.
Mojawapo ya makwazo ambayo huweza kumkuta mwanaume katika uwanja wa mapenzi ni maswali ya 'kijinga' ambayo mwanamke anaweza kumuuliza, kwa ajili ya kuangalia msimamo wake.
Japo yameitwa ya 'kijinga' lakini maswali haya yana mchango mkubwa katika mapenzi, kwani majibu yatolewayo na mwanamume kwa maswali haya ni muhimu katika mustakabali wa mapenzi. Pamoja na hayo, wapo wanaume ambao hulalamika kuwa wameshindwa kuwaelewa wanawake, hususan kuelewa maana ya yale wayazungumzayo, yakiwamo maswali yao.
Mathalani, unaweza kuwa umepanga miadi na mwanamke kwa ajili ya kutoka naye, lakini saa mbili kabla ya muda mliopanga kutoka anakwambia kuwa ameahirisha suala hilo mpaka siku nyingine, tena anakupa ujumbe huo kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu, au hata ujumbe wa sauti, badala ya kupiga simu au kukutana nawe ana kwa ana.
Kana kwamba hiyo haitoshi, unapoonekana kufadhaika mwanamke huyo huyo anaweza kukuuliza, "Kwani vipi, mbona hivi? Una nini leo? Unaonekana uko mbali kabisa kimawazo. Uko sawa lakini?" Hii inaweza kuwa saa kadhaa baada ya kuitolea nje ofa yako ya kutoka ambayo aliishaikubali awali.
Wakati mwingine unaweza kuwa umetoka naye mara kadhaa, lakini mara hii unapomwambia suala la kutoka anakuuliza "Lakini uhusiano wetu huu unaelekea wapi? Si tunapoteza muda tu lakini?"
Maswali ya aina ya kwanza hapo juu yanaonekana ni ya kijinga, kwa sababu mwanamke huyu anafahamu fika kuwa mabadiliko ya hisia zako yametokana na hatua yake ya kuahirisha mtoko katika dakika za majeruhi.
Vivyo hivyo, maswali ya aina ya kwanza yanaweza kuitwa ya kijinga, kwani mwanamke angeweza kusubiri na kuelezwa umepanga kwenda wapi na si kukurupuka na kudhani, pengine, kuwa mnakwenda mlikokwenda mara ya mwisho ambako hakukuona kwa maana.
Hata hivyo, kama kuna mtu anadhani ameishakumbana na maswali ya aina hii, asijidhanie kuwa wa kwanza wala wa mwisho, kwani mwanamke anazo njia nyingi za kumjaribu mwanaume kuangalia kama kweli anampenda na amedhamiria kuwa naye daima.
Kanuni ya msingi ya kutumia unapojikuta katika hali hii ni kumpa changamoto mwanamke, hadi kufikia hatua yeye akawa katika wasiwasi wa kukupoteza. Kwa ujumla, usikubali kila mara kuwa mtu wa kujitetea na kulazimika kutoa majibu ya kujisafisha kwa mwanamke.
Hakikisha kuwa mwanamke ndiye anayekuwa katika hali ya kuchanganyikiwa kutokana na msimamo wako, badala ya wewe kuchanganyikiwa kutokana na majibu yake, kwani wanawake hawana majibu ya moja kwa moja.
Kama, mathalani, kwa kuzingatia mfano ulioelezwa hapo juu, mwanamke ameahirisha mtoko halafu akawa anakuuliza maswali ya kijinga, basi kuna kila dalili kuwa alipokwambia ameahirisha ulifadhaika au kukasirika.
Kwa hakika karibu kila mwanaume atakuwa na mabadiliko akikataliwa mtoko, hasa kama alikuwa na maandalizi makubwa ya kimwili, kisaikolojia na kifedha, tena zaidi kama amebadilisha mawazo katika dakika za mwisho (kama wafanyavyo mara kwa mara).
Lakini hali itakuwa mbaya zaidi kama mwanamke mwenyewe anautesa moyo wake na ilikuwa iwe mara yako ya kwanza kujivinjari naye viwanja.
Lakini katika hali kama hiyo pamoja na hali nyingine ambapo mwanamke anaonesha kutokukujali kwa kadiri unavyomchukulia, unapaswa kujitokeza kama mtu asiyetetereka, ukionesha kutoshtuka, ukiendelea kujiamini. Kamwe usimwoneshe mpenzi wako, au mpenzi wako mtarajiwa, kuwa kitendo chake cha kukupuuza kimekuuma.
Baada ya kukabiliana na hali hii kwa mara ya kwanza, siku nyingine mpenzi wako (au msichana unayemfukuzia) akikupiga chini dakika za mwisho ukiwa naye ana kwa ana, hakikisha kuwa humwoneshi kuwa umefadhaishwa na hatua yake kwa namna yoyote ile na ikiwezekana waweza kumwonesha kuwa kumbe kuvuja kwa pakacha kumekuwa nafuu kwa mchukuzi, kwa kumwambia kuwa wewe pia una shughuli nyingine muhimu ya kufanya jioni au siku hiyo na kwamba amekusaidia sana.
Lakini kama kwa sababu yoyote ile mwanamke ataendelea kukuuliza maswali ya kijinga baada ya kukuumiza, mathalani akakuuliza kama hujisikii vizuri, mjibu kwamba ni kinyume cha mawazo yake, kwani kwa hakika umejisikia kutua mzigo.
Unapoyasema hayo, usionekane kukasirika, bali onesha tabasamu na kicheko, japo ndani unaweza kuwa unajihisi kuumia.
Mwache mwanamke akijiuliza umemaanisha nini hasa kwa kusema kuwa umetua mzigo, au hata kwa kuonesha kuwa hukuumia. Kumbuka kuwa msichana huyu alifahamu tangu awali kuwa asingekuwa tayari kutoka na wewe siku hiyo kwa hiyo hatua yake haikuwa ya bahati mbaya, bali ina malengo.
Kwa msichana aliyekweleza kuwa anahisi kutoka ni kupoteza muda, ni dhahiri kuwa mapenzi yake kwako yatakuwa madogo. Mwanamke anayekupenda kwa dhati hawezi kudhani kutoka na wewe ni kupoteza muda.
Lakini hata hivyo, anapokutamkia kauli hiyo nia yake ni kukuweka katika shinikizo. Kwa hiyo, kama kawaida, mgeuzie kibao kwa kuelekeza changamoto kwake. Kama, mathalani atasema, "Sitaki unipotezee muda. Kweli huna mwanamke mwingine?" Mwambie: "Mpenzi, huwezi kupoteza muda ukiwa na mimi." Maswali yake mengine yajibu kwa majibu muafaka pia.
La muhimu ambalo mwanaume anapaswa kulifahamu ni kwamba, njia nzuri zaidi ya kuishi na mwanamke ni kumfanya kila mara aendelee kuwa na shaka kuhusiana na mawazo yako, asije akautumia udhaifu wako kukunyanyasa.
Wanaume wengi hujikuta wakitumia nguvu nyingi kuwabembeleza wanawake kwa ajili ya mambo mbalimbali na kwa kufanya hivyo hujikuta wakichezewa na wanawake wasiokuwa na mapenzi ya dhati kwao.
Lakini siri kubwa ya kufanikiwa katika mapenzi ni pamoja na kumwacha mwanamke katika hali ambayo kila mara anataka kufahamu zaidi kuhusiana na msimamo wako na njia mojawapo ya kufanya hivi ni kutoa majibu muafaka kwa maswali muafaka.
Kama mwanamke unayemfukuzia hajaonesha kuvutiwa sana nawe, itakuwa rahisi kwake kukukimbia atakapobaini kuwa kumbe huna msimamo na unaweza kuyumbishwa na kufadhaishwa kwa jambo dogo, kama kuahirishiwa tarehe ya mtoko.
Lakini kama amevutiwa nawe, msimamo wako na kujiamini kwako vitampa changamoto kiasi cha kujihisi kuwa atakuwa amepata hasara kwa kumkosa mwanamume wa aina yako.
KWA mtu ambaye ndiyo kwanza anajiingiza katika ulimwengu wa mapenzi, ni dhahiri kuwa atakutana na mambo mengi ya kumkwaza, ambayo hatimaye yanaweza kumvunja moyo kuhusiana na suala zima la mapenzi. Wanaume, hususan kwa kuwa ndio wenye jukumu la kuanzisha mahusiano, hujikuta katika wakati mgumu wanapokwenda kukabiliana na wanawake, kutokana na tabia za wanawake, hasa wasichana za kutaka kujilinda.
Wanaume wengi wamekata tamaa na kubaki wakinung'unika, kutokana na kusalimu amri kwa makwazo mbalimbali yatokanayo na tabia ya asili ya mwanamke, ya kumjaribu mwanaume.
Mojawapo ya makwazo ambayo huweza kumkuta mwanaume katika uwanja wa mapenzi ni maswali ya 'kijinga' ambayo mwanamke anaweza kumuuliza, kwa ajili ya kuangalia msimamo wake.
Japo yameitwa ya 'kijinga' lakini maswali haya yana mchango mkubwa katika mapenzi, kwani majibu yatolewayo na mwanamume kwa maswali haya ni muhimu katika mustakabali wa mapenzi. Pamoja na hayo, wapo wanaume ambao hulalamika kuwa wameshindwa kuwaelewa wanawake, hususan kuelewa maana ya yale wayazungumzayo, yakiwamo maswali yao.
Mathalani, unaweza kuwa umepanga miadi na mwanamke kwa ajili ya kutoka naye, lakini saa mbili kabla ya muda mliopanga kutoka anakwambia kuwa ameahirisha suala hilo mpaka siku nyingine, tena anakupa ujumbe huo kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu, au hata ujumbe wa sauti, badala ya kupiga simu au kukutana nawe ana kwa ana.
Kana kwamba hiyo haitoshi, unapoonekana kufadhaika mwanamke huyo huyo anaweza kukuuliza, "Kwani vipi, mbona hivi? Una nini leo? Unaonekana uko mbali kabisa kimawazo. Uko sawa lakini?" Hii inaweza kuwa saa kadhaa baada ya kuitolea nje ofa yako ya kutoka ambayo aliishaikubali awali.
Wakati mwingine unaweza kuwa umetoka naye mara kadhaa, lakini mara hii unapomwambia suala la kutoka anakuuliza "Lakini uhusiano wetu huu unaelekea wapi? Si tunapoteza muda tu lakini?"
Maswali ya aina ya kwanza hapo juu yanaonekana ni ya kijinga, kwa sababu mwanamke huyu anafahamu fika kuwa mabadiliko ya hisia zako yametokana na hatua yake ya kuahirisha mtoko katika dakika za majeruhi.
Vivyo hivyo, maswali ya aina ya kwanza yanaweza kuitwa ya kijinga, kwani mwanamke angeweza kusubiri na kuelezwa umepanga kwenda wapi na si kukurupuka na kudhani, pengine, kuwa mnakwenda mlikokwenda mara ya mwisho ambako hakukuona kwa maana.
Hata hivyo, kama kuna mtu anadhani ameishakumbana na maswali ya aina hii, asijidhanie kuwa wa kwanza wala wa mwisho, kwani mwanamke anazo njia nyingi za kumjaribu mwanaume kuangalia kama kweli anampenda na amedhamiria kuwa naye daima.
Kanuni ya msingi ya kutumia unapojikuta katika hali hii ni kumpa changamoto mwanamke, hadi kufikia hatua yeye akawa katika wasiwasi wa kukupoteza. Kwa ujumla, usikubali kila mara kuwa mtu wa kujitetea na kulazimika kutoa majibu ya kujisafisha kwa mwanamke.
Hakikisha kuwa mwanamke ndiye anayekuwa katika hali ya kuchanganyikiwa kutokana na msimamo wako, badala ya wewe kuchanganyikiwa kutokana na majibu yake, kwani wanawake hawana majibu ya moja kwa moja.
Kama, mathalani, kwa kuzingatia mfano ulioelezwa hapo juu, mwanamke ameahirisha mtoko halafu akawa anakuuliza maswali ya kijinga, basi kuna kila dalili kuwa alipokwambia ameahirisha ulifadhaika au kukasirika.
Kwa hakika karibu kila mwanaume atakuwa na mabadiliko akikataliwa mtoko, hasa kama alikuwa na maandalizi makubwa ya kimwili, kisaikolojia na kifedha, tena zaidi kama amebadilisha mawazo katika dakika za mwisho (kama wafanyavyo mara kwa mara).
Lakini hali itakuwa mbaya zaidi kama mwanamke mwenyewe anautesa moyo wake na ilikuwa iwe mara yako ya kwanza kujivinjari naye viwanja.
Lakini katika hali kama hiyo pamoja na hali nyingine ambapo mwanamke anaonesha kutokukujali kwa kadiri unavyomchukulia, unapaswa kujitokeza kama mtu asiyetetereka, ukionesha kutoshtuka, ukiendelea kujiamini. Kamwe usimwoneshe mpenzi wako, au mpenzi wako mtarajiwa, kuwa kitendo chake cha kukupuuza kimekuuma.
Baada ya kukabiliana na hali hii kwa mara ya kwanza, siku nyingine mpenzi wako (au msichana unayemfukuzia) akikupiga chini dakika za mwisho ukiwa naye ana kwa ana, hakikisha kuwa humwoneshi kuwa umefadhaishwa na hatua yake kwa namna yoyote ile na ikiwezekana waweza kumwonesha kuwa kumbe kuvuja kwa pakacha kumekuwa nafuu kwa mchukuzi, kwa kumwambia kuwa wewe pia una shughuli nyingine muhimu ya kufanya jioni au siku hiyo na kwamba amekusaidia sana.
Lakini kama kwa sababu yoyote ile mwanamke ataendelea kukuuliza maswali ya kijinga baada ya kukuumiza, mathalani akakuuliza kama hujisikii vizuri, mjibu kwamba ni kinyume cha mawazo yake, kwani kwa hakika umejisikia kutua mzigo.
Unapoyasema hayo, usionekane kukasirika, bali onesha tabasamu na kicheko, japo ndani unaweza kuwa unajihisi kuumia.
Mwache mwanamke akijiuliza umemaanisha nini hasa kwa kusema kuwa umetua mzigo, au hata kwa kuonesha kuwa hukuumia. Kumbuka kuwa msichana huyu alifahamu tangu awali kuwa asingekuwa tayari kutoka na wewe siku hiyo kwa hiyo hatua yake haikuwa ya bahati mbaya, bali ina malengo.
Kwa msichana aliyekweleza kuwa anahisi kutoka ni kupoteza muda, ni dhahiri kuwa mapenzi yake kwako yatakuwa madogo. Mwanamke anayekupenda kwa dhati hawezi kudhani kutoka na wewe ni kupoteza muda.
Lakini hata hivyo, anapokutamkia kauli hiyo nia yake ni kukuweka katika shinikizo. Kwa hiyo, kama kawaida, mgeuzie kibao kwa kuelekeza changamoto kwake. Kama, mathalani atasema, "Sitaki unipotezee muda. Kweli huna mwanamke mwingine?" Mwambie: "Mpenzi, huwezi kupoteza muda ukiwa na mimi." Maswali yake mengine yajibu kwa majibu muafaka pia.
La muhimu ambalo mwanaume anapaswa kulifahamu ni kwamba, njia nzuri zaidi ya kuishi na mwanamke ni kumfanya kila mara aendelee kuwa na shaka kuhusiana na mawazo yako, asije akautumia udhaifu wako kukunyanyasa.
Wanaume wengi hujikuta wakitumia nguvu nyingi kuwabembeleza wanawake kwa ajili ya mambo mbalimbali na kwa kufanya hivyo hujikuta wakichezewa na wanawake wasiokuwa na mapenzi ya dhati kwao.
Lakini siri kubwa ya kufanikiwa katika mapenzi ni pamoja na kumwacha mwanamke katika hali ambayo kila mara anataka kufahamu zaidi kuhusiana na msimamo wako na njia mojawapo ya kufanya hivi ni kutoa majibu muafaka kwa maswali muafaka.
Kama mwanamke unayemfukuzia hajaonesha kuvutiwa sana nawe, itakuwa rahisi kwake kukukimbia atakapobaini kuwa kumbe huna msimamo na unaweza kuyumbishwa na kufadhaishwa kwa jambo dogo, kama kuahirishiwa tarehe ya mtoko.
Lakini kama amevutiwa nawe, msimamo wako na kujiamini kwako vitampa changamoto kiasi cha kujihisi kuwa atakuwa amepata hasara kwa kumkosa mwanamume wa aina yako.
0 Maoni