Usitarajie Kila Kitu Kiwe Shwari Katika NDOA bila Misukosuko.
ππππππππ
Usitarajie Kushiba,Kuvaa,Kuoga Bila ya Kukosa cha Kutia Kinywani Au Kuvaa Mwilini ni jambo la Kawaida Katika NDOA.
ππππππππ
Usitarajie Aliyekuoa au Uliyemuoa Awe Mkamilifu Utakavyo Wewe! Bila Shaka Utie Akilini Kwamba Chochote Kizuri kina Ubaya Na Kinyume Chake.
ππππππππ
Usitarajie Kubembelezwa katika Ndoa Bila maneno Makali Bila Manung'uniko katika Ndoa. Bila Shaka Kuna Kusutwa,Kupigwa,Kufukuzwa na Hata Kuchukiwa.
πΆπΆπΆπΆπΆπΆπΆπΆ
Usitarajie Vyote Katika NDOA Ni vyenye Kukufurahisha kuna Vile Vya Kuhuzunisha Kukutia Majonzi Kukupa Mihangaiko Mfadhaiko na Kukutupa Katika Lindi La Mawazo.
ππππππππ
Usitarajie Kupata Mzuri Safi,Mwenye Hekima Na Busara Katika Ndoa. Kuna Wenye Hasira Bila Busara Wenye Midomo Mikali Mno Wenye Kupungukiwa Kwa Uwezo WaKutafakari.
πΆπΆπΆπΆπΆπΆπΆπΆ
Ndo Maana NDOA ni Chuo Ni Ibaada Na Kila Ibaada Inataka Uvumilivu Wa Hali Ya Juu Mno.
πΉπΉπΉπΉπΉπΉπΉπΉ
*Sote Tuvumilie Katika NDOA zetu. ALLAAHο·» atupe Moyo Wenye Kusubiri.*

0 Maoni