UNA TATIZO HILI NDIYO MAANA MPENZI WAKO HAKUPIGII SIMU MARA KWA MARA, KILA SIKU NI WEWE TU WA KUMPIGIA!


UNA TATIZO HILI NDIYO MAANA MPENZI WAKO HAKUPIGII SIMU MARA KWA MARA, KILA SIKU NI WEWE TU WA KUMPIGIA!

Nijambo la kawaida kumsikia mtu akilalamika kuwa mpenzi wangu, mume au hata mke wangu huwa hanipigii simu wala kunitumia meseji mara kwa mara, kila wakati nilazima nimuanze mimi, mtu analalamika na kujuiona kama vile hapendwi. Mara nyingi hii hutokea kwa wanawake na inauma sana kama kila siku wewe unakua mtu wa kumtafuta mpenzi wako, anakua hajali na unajiona kama unajipendekeza.

Ulishawahi kuhisi hivyo, sasa wakati mwingine kweli inawezekana hakupendi, anakuchukulia poa kwakua anaona unampenda zaidi. Lakini wakati mwingine sio hivyo, mara nyingi na kwa idadi kubwa ya watu ambao huniomba ushauri kuhusu suala hili tatizo ni kwao hao wanaopiga simu mara kwa mara. Kwamba wewe ambaye unajiona kama unapenda zaidi kuliko mwenza wako ndiyo mwenye tatizo na si huyo unayeona hakujali.

Tatizo kubwa nikuwa humpi muda mpenzi wako wa kukumiss mpaka kukupigia simu. Labda nifafanue kidogo katika maisha ya kawaida watu hupigiana simu wakiwa na shida flani, hasa wanaume, mpaka kuwe na kitu falani ndiyo hupiga simu, mimi binafsi kuna baadhi ya ndugu zangu naweza kukaa mwaka bila kuongea nao, sio kwamba siwapendi hapana lakini sina cha kuongea nao.

Lakini katika mapenzi watu hupigiana simu kwakua wanatamaniana, wamemisiana, unapokaa na kujihisi mpweke unaona njia rahisi ya kupata faraja ni kwa kumpigia simu mpenzi wako. Huwezi kumpigia tu kama hujamkumbuka, kama huna cha kuongea hapana nilazima umkumbuke. Sasa kuna watu ambao hawakupi hata muda wa kuwamiss na kuwakumbuka, kwamba kila wakati anakupigia simu mpaka unamchoka.

Labda twende kwenye mfano huu, asubuhi umeamka mapema kabisa unampigia mpenzi wako simu kumjulia hali, mnasalimiana mnaongea yanaisha, hapa katikati unamtumia meseji mbili tatu anakujibu. Mchana wewe wewe unampigia simu na kumjulia hali, kumuuliza kama kala au la, jioni nako unampigia simu kama katoka kazini au la, usiku kabla ya kulala husubiri hata akupigie unakua na kiherehere unapiga tena.

Sasa ndugu yangu umekua kutwa mara tatu kama dozi ya Malaria unataka yeye akumiss saana
Kama ukipata mtu mpya hili lizingatie....
https://www.facebook.com/allaboutrelationshipandlife/

Chapisha Maoni

0 Maoni