JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 6

INAENDELEA HAPA: Kipindi Mr. Brown anampiga mke wake Mrs. Brown ghafla wakatokea wazazi wa Mr. Brown ambao ni wakwe wa Mrs. Brown walikwenda kuwatembelea wakakuta kuna vurugu kwa watoto wao walichokifanya wazazi wale waliamua ugomvi na kuwaweka chini na kuwasikiliza kwa umakini watoto wao chanzo cha wao kugombana ni nini? Wakaanza kuelezea ilivyokua. Wazazi wa Mr. Brown wakatumia busara na kuwasihi wasigombane na wakawapatanisha watoto wao pale pale Mr na Mrs. Brown wakamaliza tofauti zao wakawa na amani wakajumuika pamoja na wazazi wao mpaka ilipofika jioni wale wazazi wakaondoka huku nyuma Mr na Mrs. Brown walikaa na kujadili njia nyingine ya kumsaidia binti yao Jenifer aweze kuendelea na masomo shule wakaona ni bora wamtafutie tu binti yao shule nyingine ili aweze kuendelea na masomo yake, baada ya siku kadhaa Mr. Brown alijitahidi kuhangaikia shule ili aweze kumpeleka binti yake JENIFER aweze kuendelea na masomo akiwa na dhamira ile ile aliyokua nayo tangu awali kuwa binti yao JENIFER wakimsomesha
baadae atakuja kuwasaidia katika maisha yao, mungu alisaidia Mr. Brown akajitahidi akafanikiwa kumpatia nafasi binti yake JENIFER katika shule moja iitwayo KILIMANJARO SECONDARY SCHOOL na binti yao akajiunga na shule hiyo akaendelea na masomo yake. JENIFER alipokua shuleni hapo tabia yake chafu haikubadilika aliendelea na tabia yake ile ile ya kua na marafiki ambao tabia zao zilikua ni chafu na ikafikia hatua JENIFER akawa anamahusiano ya kimapenzi na waalimu wa shuleni hapo tena kwa kuwachanganya alikua anatembea na MWALIMU MKUU (head master), MWALIMU MKUU MSAIDIZI (Second master) na MWALIMU WA TAALUMA (Academic master) tena bila ya walimu hao kutofahamu kama wanachangia penzi moja kwa binti huyo, Sasa siku moja Mwalimu mkuu wa Shule hiyo ambae ni mpenzi wake JENIFER alimuita JENIFER ofisini kwake na kuanza kumshika shika ofisini hatimae wakafanya nae tendo chafu la ngono ndani ya ofisi na hawakufunga mlango wa ofisi hiyo, ghafla Mwalimu mkuu msaidizi
akafungua ule mlango wa ofisi ya mwalimu mkuu, alikua anampelekea ma faili mwalimu mkuu alipovamia akamkuta mwalimu mkuu na JENIFER wakiwa katika tendo, mwalimu mkuu msaidizi alishtuka sana kuona vile hakuongea kitu alitoka nje haraka.

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 5

 INAENDELEA HAPA:
Baada ya kuvutana sana kati ya Mwalimu mkuu na Mr. Brown ofisini ikabidi mwalimu mkuu akubali kuwa mpole na kurudisha pesa japo sio zote ilibidi mwalimu mkuu atoe nusu ya pesa zilizolipwa, Mr. Brown alilipa ada Shilingi laki moja na nusu ikabidi mwalimu mkuu atoe nusu ya pesa hizi Shilingi elfu sabini na tano na kumpa Mr. Brown. Mr. Brown akapokea zile pesa Shilingi elfu Sabini na tano akamchukua binti yake JENIFER wakaondoka na kuelekea nyumbani kipindi wapo njiani wanaelekea nyumbani, Mr. Brown alikua na hasira sana akamwambia binti yake JENIFER "We mtoto leo tukifika tu nyumbani chukua nguo zako na uondoke nyumbani kwangu sitaki kukuona, mshenzi wewe!". Walipofika nyumbani tu Mr. Brown akaanza kumuhadithia mke wake Mrs. Brown yaliyotokea shuleni kuhusu binti yao JENIFER na akamwambia Mrs. Brown kuwa hataki hata kumuona aondoke nyumbani kwake lakini kwa maamuzi haya ya Mr. Brown mke wake Mrs. Brown hakuafikiana nayo akamwambia mume wake
"SASA MUME WANGU UNAMFUKUZA MTOTO AENDE WAPI WAKATI HAPA NDIO KWAO, UNADHANI ATAENDA WAPI? KAMA MAJI YAMEISHAMWAGIKA MAKOSA NDIO KISHAFANYA HAKUNA JINSI NI KUMSAMEHE NA TUKAE TUSHAURIANE TUJUE TUNAFANYAJE MUME WANGU PUNGUZA HASIRA". Mr. Brown akamjibu "HAIWEZEKANI MIMI SITAKI HATA KUMUONA HUMU NDANI AONDOKE SITAKI KUMUONA". Mrs. Brown nae akamjibu "KAMA UNATAKA HUYU BINTI AONDOKE HUMU NDANI BASI JUA NITAONDOKA NAE SIWEZI KUKUBALI BINTI YANGU AONDOKE AKAPATE SHIDA WAKATI KWAO ANAPO, UKIMFUKUZA JUA NAMIMI NAONDOKA HUMU NDANI" Baada ya Mrs. Brown kumuambia Mume wake Mr. Brown maneno hayo ghafla Mr. Brown alisema kwa sauti kali ya juu "SAWA MKITAKA MUONDOKE WOTE, SIWEZI KUFUGA UPUMBAVU KAMA UNAONA NAMUONEA MTOTO WAKO MFUATE MUONDOKE WOTE PUMBAVU!". Mrs Brown akamjibu "EH E! TAFADHALI BABA WEE, USINITUKANE NGOJA TUKUPISHE UBAKIE NA NYUMBA YAKO SIO UNIFOKEE. MPUMBAVU MWENYEWE!. Ghafla Mr. Brown alikurupuka na kumvamia mke wake Mrs. Brown na kuanza kumpiga makofi huku akimwambia
"YANI WEWE UNADIRIKI KUNIAMBIA MIMI MPUMBAVU, WAKATI JENIFER KAFANYA MAKOSA DHAHIRI. HIVI MIMI NINAVYOHANGAIKA KUTAFUTA PESA ZA KUMSOMESHA HALAFU ANALETA UPUMBAVU UNAFURAHIA ETI EEH!"

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 4

 INAENDELEA HAPA: Mwalimu KABAVAKO aliwachapa kila mmoja fimbo nne nne, kisha akawarudisha ofisini kwa mwalimu mkuu walipofika ofisini kwa mwalimu mkuu, mwalimu mkuu aliwaambia inabidi awape adhabu ya kukaa nyumbani mpaka uongozi wa shule utakapo kaa kikao na kuwafikiria na kujadili kosa lao ndio wafanye maamuzi ya kuwasamehe au kutowasamehe. Mr. Brown baba yake na JENIFER alijitahidi sana kumbembeleza mwalimu mkuu awasamehe ili waendelee na masomo lakini mwalimu mkuu alikataa katu katu na akamwambia Mr. Brown kuwa "MZEE KOSA WALILOFANYA HAWA WATOTO NI KUBWA SANA TENA AFADHALI YA HAWA WENGINE KULIKO HUYU BINTI YAKO JENIFER, JENIFER KWANZA HANA HESHIMA KADIRIKI KUMSINGIZIA MWALIMU WANGU KUWA KAMTONGOZA WAKATI SIO KWELI HUONI KAMA HUYU MTOTO ANAWEZA KUJA KUTUCHAFULIA SIFA YA SHULE YETU? NI BORA NIWASAMEHE HAWA WOTE LAKINI KWA BINTI YAKO JENIFER SIWEZI KUMSAMEHE" ghafla mwalimu mkuu akabadilisha mawazo pale pale akawaambia wale rafiki zake na JENIFER "NYIE NIMEWASAMEHE NENDENI NYUMBANI MKAVAE NGUO ZA SHULE NA MJE DARASANI MUENDELEE NA MASOMO ILA JENIFER SINTOWEZA KUMSAMEHE SAWA?!" wale wanafunzi watatu ambao ni rafiki zake JENIFER walifurah na hawakuamini kama wamesamehewa wakamshukuru sana mwalimu mkuu na wakamuahidi kuwa hawatorudia tena, wakaondoka ofisini na kuelekea majumbani kwao kuvaa nguo za shule. Huku ofisini mwalimu mkuu akanyanyua simu yake ya mezani akampigia Secretary wake na kumuamuru achapishe barua ya kumsimamisha shule mwanafunzi wake JENIFER. Mr. Brown alijitahidi sana kumbembeleza mwalimu mkuu amsamehe binti yake mpaka machozi yakawa yanamtoka Mwalimu mkuu akamwambia Mr. Brown "MZEE HILI NATOA FUNDISHO ILI BINTI YAKO AJIFUNZE SIWEZI KUMSAMEHE MTOTO MSHENZI SANA HUYU" Mr. Brown alimbembeleza sana mwalimu mkuu lakini mwalimu mkuu alimkatalia katu katu kumsamehe JENIFER na akawaomba Mr. Brown na Binti yake JENIFER watoke nje ya Ofisi wasubirie barua ya kusimamishwa shule binti yao. Baada ya muda Secretary alimaliza kuchapa barua na kuipeleka ofisini kwa mwalimu mkuu, mwalimu mkuu akamwita kiranja mkuu wa shule akamwambia aende kupiga kengere ya dharura ili wanafunzi wote wakusanyike mstarini aitoe barua ile hadharani mbele za wanafunzi. Kengere ilipigwa wanafunzi wote wakatoka madarasani na kuelekea mstarini wakakusanyika wanafunzi wote na walimu wote wa shule hiyo, mwalimu mkuu akaanza kuelezea yote yaliyojiri kwa JENIFER na kuwajulisha wanafunzi kuwa kasimamishwa shule baada ya hapo wakateuliwa walimu watatu wamchape fimbo JENIFER kila mwalimu amchape fimbo tatu, kisha wanafunzi wakaruhusiwa waende madarasani kuendelea na masomo yao. Mr. Brown alijisikia aibu sana kwani binti yake JENIFER alichofanya ni kitu cha ajabu hivyo alikua na hasira sana kilichomuumiza ni Ada aliyoitoa shuleni hapo ya kumlipia binti yake akifikiria jinsi alivyoipata pesa katika mazingira magumu ilimradi binti yake asome lakini JENIFER yote hakujali, sasa kivumbi kikaanza kwa Mr. Brown na Mwalimu mkuu, Mr. Brown akaanza kudai pesa ya ada ya mwaka aliyolipa shule akataka arudishiwe pesa yake ukaanza mzozo ofisini kati ya Mwalimu mkuu na Mr. Brown hatimae wakaanza kushikana mashati ofisini, Mr. Brown anataka pesa mwalimu mkuu anasema hatoi pesa ikawa vurumai ofisini

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 3

INAENDELEA HAPA:
Ilipofika kesho yake asubuhi siku ya Ijumaa tatu JENIFER na baba yake Mr. Brown walifunga safari mpaka shule, walipofika shuleni hapo moja kwa moja wakaenda mpaka ofisi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo (HEAD MASTER) walipofika ofisini kwa mwalimu mkuu wakamuomba JENIFER atoke nje na aelekee mstarini baada ya hapo aende darasani kusoma. JENIFER akatoka nje na kuelekea mstarini huku ofisini akabakia mwalimu mkuu na Mr. Brown wakizungumza. Mr. Brown alimuelezea kwa kirefu mwalimu mkuu kuwa kuna mwalimu wake hapo shuleni anaitwa MWL. KABAVAKO anamtaka binti yake kama alivyoelezwa na binti yake JENIFER, baada ya mwalimu mkuu kuambiwa vile alichokifanya akamtafuta kiranja wa shule akamtuma aende kumuita JENIFER pamoja na huyo Mwalimu KABAVAKO wafike ofisini hapo kwa mwalimu mkuu. Yule kijana ambae ni kiranja akaenda kuwaita JENIFER na Mwalimu KABAVAKO walipofika ofisini mwalimu mkuu akamuomba JENIFER aelezee ilivyokua kuhusu mwalimu KABAVAKO. JENIFER akaanza kuelezea kama alivyowaelezea wazazi wake kuwa mwalimu KABAVAKO anamtaka kimapenzi lakini yeye hamtaki na amekua anamtesa sana shuleni hapo, na amemuahidi kuwa atafanya kila njia ili amfukuzishe shule pia kuna wanafunzi aliwakamata disco usiku mwalimu KABAVAKO akamuahidi Jenifer kuwa atamuingiza nayeye katika hilo kosa la hao wanafunzi ili wafukuzwe wote shule. Ndivyo JENIFER alivyojitetea kwa kusema haya mbele ya baba yake Mr. Brown, mwalimu mkuu na mwalimu KABAVAKO. Mwalimu kabavako alipigwa na butwaa akabakia anashangaa kutokana na maneno aliyosingiziwa lakini alikua ni mwenye busara na subira akamuacha JENIFER azungumze mpaka alipomaliza ikafika zamu yake mwalimu KABAVAKO ajielezee alichokifanya mwalimu kabavako akamuuliza swali JENIFER "JENIFER WEWE HAPA SHULENI UNA MARAFIKI?" Jenifer akamjibu "NDIO NINAO" mwalimu KABAVAKO akamwambia "UNAWEZA KUNITAJIA MARAFIKI ZAKO WATATU MUHIMU AMBAO NI WAKARIBU SANA?!" Jenifer akaanza kuwataja marafiki zake watatu ambao ndio yupo nao karibu sana na katika hao marafiki watatu aliowataja JENIFER ndio wale ambao mwalimu KABAVAKO aliwakamata wako wote na JENIFER usiku, baada ya hapo mwalimu KABAVAKO akamuuliza baba yake na JENIFER "MZEE SIKU YA IJUMAA MOSI BINTI YAKO JENIFER ALILALA NYUMBANI?!" Baba yake na JENIFER akajibu "MWALIMU MBONA SIKUELEWI TUNAULIZANA MASWALI KAMA TUPO KITUO CHA POLISI?" mwalimu KABAVAKO akamjibu "MZEE PUNGUZA JAZBA MIMI NINAKUULIZA HIVI NINA MAANA YANGU" baba yake na Jenifer ikabidi amjibu mwalimu "KILA SIKU YA IJUMAA MOSI MWANANGU HUWA ANATOKA ANAENDA KUJISOMEA NA WENZAKE USIKU KUCHA ASUBUHI ANARUDI NYUMBANI" baada ya mwalimu KABAVAKO Kumuuliza maswali JENIFER na baba yake kisha akatoka nje na kumtafuta mwanafunzi kisha akamuagiza yule mwanafunzi aende ofisi kuwaita wale wanafunzi watatu aliowakamata wakiwa Club usiku pamoja na JENIFER, yule mwanafunzi akaenda kuwaita wale rafiki zake na JENIFER walikuwa wamevaa mavazi yao ya nyumbani waliyokamatwa nayo wakaelekea mpaka ofisi ya mwalimu mkuu. Walipofika ofisini mwalimu KABAVAKO akawauliza "NYIE WANAFUNZI MNAMJUA HUYU MWANAFUNZI MWENZENU?" wakajibu "NDIO MWALIMU TUNAMJUA ANAITWA JENIFER" akawauliza tena "KWANINI NYIE MMEKUJA SHULENI MKIWA MMEVAA HIZO NGUO ZA NYUMBANI TENA FUPI?" wale wanafunzi wakajibu "MWALIMU WEWE SI ULITUKAMATA SIKU YA IJUMAA MOSI USIKU CLUB UKATUAMBIA TUJE LEO OFISINI KWAKO NA HIZI NGUO PAMOJA NA WAZAZI WETU?" mwalimu KABAVAKO akawauliza tena "NILIPO WAKAMATA HIYO SIKU YA IJUMAA MOSI MLIKUA NYIE NYIE WATATU PEKE YENU AU?" wakajibu "HAPANA MWALIMU TULIKUA PAMOJA NA JENIFER" pale pale JENIFER nguvu zikamuishia akajua tayari kishakamatwa hana jinsi akaanza kulia ofisini kwa mwalimu mkuu. Mwalimu mkuu akamwambia JENIFER "JENIFER TAFADHALI USINIFICHE NIELEZE UKWELI UKINIDANGANYA NAWEZA KUKUCHAPA HAPA MBELE YA BABA YAKO NA NITAKUFUKUZA SHULENI KWANGU, NIELEZE UKWELI SI UNAONA WENZAKO WAMENIELEZA UKWELI? HAYA NAWEWE NIELEZE UKWELI WAKO, MWALIMU KABAVAKO ALIKUKAMATA CLUB KWELI?" JENIFER akajikuta anasema ukweli "NDIO MWALIMU ALINIKAMATA JUZI IJUMAA MOSI USIKU NIKO NA HAWA MARAFIKI ZANGU CLUB" mwalimu mkuu akamuuliza tena "NA JE, NIKWELI MWALIMU KABAVAKO AMEISHAWAHI KUKUTONGOZA?" JENIFER akakosa jibu akakaa kimya, ghafla JENIFER akasema "BABA NAKUOMBA UNISAMEHE NILIKUDANGANYA MWALIMU HAJAWAH KUNITONGOZA ILA NILITAKA NIJITETEE UKWELI NIKWAMBA ALITUKAMATA CLUB USIKU" pale pale Mr. Brown nguvu zilimuishia akamwambia mwalimu KABAVAKO "MWALIMU NISAMEHE MIMI KWA YOTE HAYA, KUMBE HUYU MTOTO NI MUONGO SINA LA KUSEMA NAOMBA MUMPE ADHABU YOYOTE ILE NIKO TAYARI, MSHENZI SANA HUYU MTOTO" mwalimu mkuu akamwambia mwalimu KABAVAKO atoke nje na wale wanafunzi watatu pamoja na JENIFER akawachape fimbo kisha arudi nao ofisini kwake. Mr. Brown akabakia na mwalimu mkuu wanaongea!

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 2

INAENDELEA HAPA: Baada ya JENIFER na wenzake kukamatwa na mwalimu na kupewa adhabu hiyo ya kwenda na wazazi wao shuleni siku ya Ijumaa tatu na kupelekea kupoteza mudi ya kuendelea kufurah usiku huo ikawabidi waondoke kabisa sehemu hiyo ya CLUB usiku huo huo na kwenda kulala kwenye chumba cha rafiki yao CHRISTINA waliekuwa nae katika kundi lao usiku huo, ilipofika kesho yake siku ya ijumaa pili asubuhi kila mtu alirejea nyumbani kwao huku wakiwa na sura za hudhuni na mawazo kibao kichwani wakijiuliza itakuaje kesho yake ambayo ni siku ya Ijumaa tatu wanatakiwa waende shule na wazazi wao?!. Jenifer alipofika kwao moja kwa moja alielekea chumbani kwake na kujilaza kitandani huku akiwa na mawazo kibao hata chakula hakuweza kula siku hiyo muda wote alikua kajifungia chumbani analia. Ghafla akasikia mlango wa chumbani kwake unafunguliwa aliposhtuka akamuona mama yake Mrs. Brown. Mrs. Brown alimsogelea binti yake Jenifer kuanza kuzungumza nae kama ifuatavyo:-

MRS. BROWN:
 "Jenifer binti yangu mbona unaonekana leo hauko sawa, nini tatizo mwanangu?! Na mbona unalia?

JENIFER:
 "Hapana mama, wala usijali hamna kitu chochote naomba uwe na amani mama yangu, niko sawa tu!"

MRS. BROWN:
 "Jenifer mwanangu lazima kutakuwa kuna kitu ila unaficha. Mwanangu nakuomba unieleze usinifiche niambie tu mwanangu wala usiogope"

JENIFER:
 "Mama wala usijali hakuna kitu chochote kile"

MRS. BROWN:
 "Sidhani binti yangu kama kweli hakuna tatizo sasa mbona unalia, Au umepata ujauzito?!

JENIFER:
 "Mama bora ningekua nina ujauzito ila kwa hiki kilichonipata mama yangu najuta tena najuta hata sijui kwanini mlinipeleka shule mama yangu"

MRS. BROWN:
 "Mwanangu mbona unasema hivyo kwani kuna tatizo limetokea shule?!

JENIFER:
 "Ndio mama, kuna mwalimu shuleni alinitongoza nikamkatalia sasa kila siku huwa ananichapa fimbo bila makosa na ananitesa sana shule na kaniahidi kuwa atanitafutia kosa lolote la uongo ili nifukuzwe shule anikomoe na juzi siku ya Ijumaa kuna wanafunzi kawakamata usiku CLUB akawaambia kuwa atawafukuza shule sasa kaniambia namimi ataniingiza katika hilo kosa la hao wanafunzi kesho shuleni ili nifukuzwe namimi"
MRS. BROWN:
 "Haiwezekani mwanangu wewe nyamaza acha kulia tumsubiri baba yako aje nimuelezee ikiwezekana kesho akupeleke shule akamkomeshe huyo mwalimu, wala usiwaze sana mwanangu Jenifer looooo, huyo mwalimu hana hata aibu"

Baada ya Jenifer kutumia uongo wa kumdanganya mama yake Mrs. Brown kwa dhumuni la kujitetea kutokana na kosa alilolifanya usiku wa jana yake walipokutwa na mwalimu wao wa shule CLUB ikamlazimu kumpa kesi ya uongo yule mwalimu kwa wazazi wake ili wasimuone yeye anamakosa. Mama yake na Jenifer Mrs. Brown alihamaki na kuingiwa na hasira akawa anamsubiria mume wake arudi ili amuelezee kilichotokea. Ghafla baba yake na Jenifer Mr. Brown akaingia nyumbani kwake na kumkuta mke wake Mrs. Brown akiwa na binti yao Jenifer, Jenifer alipomuona baba yake Mr. Brown akaanza kuangua kilio huku akisema "BABA NAJUTA MIMI MWANAOO, NAJUTA BABA HIVI KWANINI ULINIPELEKA NIKASOME ILE SHULE BABA YANGUUUUUU" Jenifer alikua analia huku akitoa sauti kubwa ya kumlalamikia baba yake. Mr. Brown alipigwa na butwaa hakujua nini kinachoendelea ikabidi akae chini na kumuuliza mke wake "MKE WANGU NINI KIMEMPATA BINTI YETU JENIFER?" Mrs. Brown akamjibu mume wake "MUME WANGU NENDA KWANZA KAKOGE KISHA ULE HALAFU NDIO NIKUELEZEE KILICHOTOKEA" Mr. Brown nae akamjibu "HAPANA MKE WANGU NIELEZEE KWANZA NIJUE TATIZO NINI?". Mrs. Brown ikabidi aanze kumuhadithia kama alivyohadithiwa na binti yao Jenifer kuwa kuna mwalimu wa shule alimtongoza binti yao akamkataa sasa huyo mwalimu anamtesa sana Jenifer shuleni na kamuahidi atamfanyia njama yoyote ili binti yao afukuzwe shuleni. Pale pale Mr. Brown nayeye akapandwa na hasira akamnyamazisha binti yake Jenifer na kumwambia "JENIFER BINTI YANGU NYAMAZA, KESHO IJUMAA TATU ASUBUHI TUTAKWENDA WOTE MPAKA SHULENI KWENU UKANIONESHE HUYO MWALIMU. ATANITAMBUA" baada ya hapo wakatawanyika Jenifer akaingia chumbani akaanza kushangilia peke yake kimya kimya akiwa na imani kuwa kishamaliza kesi aliyokuwa nayo na akawa na furaha tele akaendelea kufanya mambo yake kama kawaida.

JAMANI MIE UKAHABA SASA BASI" PART 1

 AMANI MIE UKAHABA SASA BASI NI HADITHI INAYOMUHUSU BINTI WA KITANZANIA ALIETUNUKIWA UZURI WA ASILI NA MVUTO WA KIPEKEE ALIOJAALIWA NA MUNGU AMA HAKIKA UZURI ALIOKUWA NAO ULIKUWA NI KISHAWISHI TOSHA KWA MWANAUME YOYOTE ALIEMTAZAMA BINTI HUYU NA KUTAMANI KUWA NAE KUTOKANA NA MVUTO ALIOKUWA NAO BINTI HUYU ANAITWA JENIFER NA AMEZALIWA KATIKA FAMILIA DUNI YA MR. BROWN NA MRS. BROWN YENYE WATOTO WATATU (3). AMBAO NI PETER, JOSEPH NA JENIFER NA KATIKA WATOTO HAWA WATATU MWANAMKE ALIKUA NI JENIFER PEKE YAKE NA NDIE ALIKUA MTOTO WA KWANZA KUZALIWA KATIKA FAMILIA HII YENYE WATOTO WATATU AMBAPO PETER NA JOSEPH WALIKUA NI WADOGO ZAKE NA JENIFER NA WALIKUWA BADO NI WADOGO SANA. NA WAZAZI WA JENIFER MR. BROWN NA MRS. BROWN WALITOKEA KUMPENDA SANA BINTI YAO JENIFER KWANI NDIO MTOTO PEKEE WA KIKE HIVYO WALIONESHA UPENDO MWINGI KWA BINTI YAO KWA KUMTIMIZIA MAHITAJ YOTE MUHIMU NA KUMPA KILA ALICHOKITAKA BINTI YAO ILI WAMRIDHISHE NA KUHAKIKISHA WANAMPA MALEZI BORA NA KUJENGA UPENDO IMARA KWA BINTI YAO. KUTOKANA NA HALI YA NGUMU YA MAISHA ILIYOKUWEPO KATIKA FAMILIA HIYO YA MR. BROWN NA MRS. BROWN, WAZAZI HAWA WALIKAA NA KUJADILI NJIA SAHIHI YA KUWEZA KUKABILIANA NA UMASIKINI WALIO NAO NA KUWEZA KUJIKWAMUA KIMAISHA WAKAPATA WAZO LA KUMPELEKA SHULE BINTI YAO JENIFER ILI HAPO BAADAE AJE KUWASAIDIA WAZAZI WAKE KUPITIA ELIMU ATAKAYOIPATA SHULE HIVYO WAZAZI WAKAKUBALIANA NA KUANZA MIPANGO YA KUMUANDIKISHA SHULE BINTI YAO ILI AANZE KUSOMA, WAZAZI WA JENIFER WALIJITAHIDI KUTAFUTA PESA KWA HALI NA MALI IKAPELEKEA WAZAZI WA JENIFER KUJIUNGA NA KAMPUNI ZINAZOTOA MIKOPO YA FEDHA LENGO KUPATA PESA WAWEZE KUMTIMIZIA MAHITAJI BINTI YAO AWEZE KUANZA SHULE. MUNGU ALILETA KHERI KWA WAZAZI HAO NA KUFANIKISHA KUIPATA PESA YA KUMPATIA BINTI YAO KWA AJILI YA MATUMIZI MADOGO MADOGO YA SHULE NA BINTI YAO AKAFANIKIWA KUANZA ELIMU YA MSINGI AKASOMA DARASA LA KWANZA MPAKA DARASA LA SABA LAKINI ALIPO MALIZA DARASA LA SABA MATOKEO YAKE HAYAKUA MAZURI HIVYO HAKUWEZA KUCHAGULIWA KATIKA SHULE ZA SEREKALI KWA AJILI YA KUENDELEA NA ELIMU YA SEKONDARI LAKINI WAZAZI WA JENIFER HAWAKUKATA TAMAA NA WALIENDELEA KUWA NA MOYO WA KUMSAIDIA BINTI YAO JENIFER KWA VYOVYOTE VILE MPAKA WAONE MWISHO WAKE KWANI MALENGO YAO BINTI YAO ASOME MPAKA DARAJA LA JUU AFIKE MPAKA CHUO KIKUU, BAADA YA JENIFER KUMALIZA ELIMU YA MSINGI NA HAKUFANIKIWA KUFANYA VIZURI KATIKA MITIHANI YAKE IKABIDI WAZAZI WAJIPANGE UPYA KUTAFUTA ADA YA KUMLIPIA BINTI YAO ILI AWEZE KUJIUNGA NA ELIMU YA SEKONDARI KWA DHUMUNI LA KUHAKIKISHA BINTI YAO JENIFER ANAENDELEA NA ELIMU. MUNGU HAKUITUPA FAMILIA HII YA MR NA MRS. BROWN ALIWAJAALIA WAKAFANIKIWA KUIPATA PESA YA KUMLIPIA ADA BINTI YAO NA WAKAMUANDIKISHA KATIKA SHULE YA KULIPIA YA SEKONDARI ILIYOFAHAMIKA KWA JINA LA "GARDEN SECONDARY SCHOOL" JENIFER ALIJIUNGA NA SHULE HII NA KUANZA ELIMU YAKE YA SEKONDARI LAKINI KAMA ILIVYO KWA VIJANA WENGI WA KISASA KUTOFAHAMU UMUHIMU WA ELIMU NA KUSHINDWA KUJUA NINI WANAPASWA KUKIFANYA PINDI WANAPO KUWA SHULE NDIVYO ILIVYOKUWA KWA JENIFER. JENIFER HAKUJUA UMUHIMU WA ELIMU NA HAKUONA JUHUDI ZA WAZAZI WAKE KWAKE ZA KUTAFUTA PESA KWA AJILI YA KUMLIPIA ADA ILI AJE KUWASAIDIA BAADAE NA KUWASAIDIA WADOGO ZAKE PETER NA JOSEPH. KIPINDI JENIFER ALIPOKUA SHULENI HAPO AKIENDELEA NA ELIMU YA SEKONDARI TABIA YAKE ILIBADILIKA AKAWA ANAUTUMIA MUDA WAKE MWINGI WA SHULE KUJICHANGANYA NA MARAFIKI AMBAO HAWAKUWA NA MSAADA MZURI KWAKE NA WAKATI MWINGINE ALIKUA AKIAGA KWAO ANAKWENDA SHULE LAKINI ALIKUA HAFIKI SHULE ALIKUA ANAKWENDA KWA MARAFIKI ANASHINDA NA KURUDI NYUMBANI WAZAZI WAKE HAWAKUJUA KINACHOENDELEA KWA BINTI YAO. WAKATI MWINGINE JENIFER ALIKUWA NI MTU WA KUPENDA SANA KWENDA KWENYE KUMBI MBALI MBALI ZA STAREHE WAKATI ALIKUA ANATOKA NYUMBANI KWAO USIKU AKIWAAGA WAZAZI WAKE KUWA ANAKWENDA KWA MARAFIKI ZAKE ANAOSOMA NAO WANAKWENDA KUKESHA WAKISOMA NA KUJADILIANA YALE WALIYOFUNDISHWA SHULENI, WAZAZI WA JENIFER HAWAKUWA NA KIPINGAMIZI KWA BINTI YAO WALIKUA RIDHWAA KUKUBALIANA NA KILA ANACHOHITAJI BINTI YAO ILI MRADI KUMRIDHISHA NA KUMFANYA AWE HURU ILI MWISHO WA SIKU AWEZE KUTIMIZA NDOTO ZA WAZAZI WAKE HIVYO WAZAZI WALIKUA WAKIMPA RUHUSA BINTI YAO ATOKE USIKU WAKIDHANI ANAENDA KUSOMA NA WENZAKE KUMBE JENIFER ALIKUA ANATUMIA MUDA HUO KUTOKA NA KWENDA CLUB (KUMBI ZA STAREHE) NA MARAFIKI ZAKE WANAENDA KUJIRUSHA NA ALIKUA ANARUDI NYUMBANI KWAO KESHO YAKE ASUBUHI, NA ILIKUA KILA IKIFIKA SIKU YA IJUMAA MOSI NDIO ANATOKA USIKU NA WENZAKE, SIKU MOJA KAMA KAWAIDA YAKE JENIFER NA WENZAKE WAMETOKA NA KWENDA KWENYE KUMBI ZA STAREHE HUKU NYUMBANI WAZAZI WANAJUA WATOTO WAO WAMEENDA KATIKA MASOMO YAO KAMA ILIVYOZOELEKA, KIPINDI WAPO CLUB KUNA MWALIMU WAO WA SHULE ALIKUWEPO KATIKA UKUMBI HUO WA STAREHE NA AKAKUTANA NA KUNDI HILI LA WAKINA DADA KAMA WANNE AKIWEMO NA JENIFER WAKIWA WAMEVAA MAVAZI MAFUPI YA AJABU KAMA MACHANGUDOA WANAOJIUZA, YULE MWALIMU WAO ALICHOKIFANYA AKAWAITA KISHA AKAWAAMBIA "NAOMBA SIKU YA IJUMAA TATU MKIFIKA SHULE CHA KWANZA NAOMBA NIWAKUTE OFISINI KWANGU KAMA MLIVYO WANNE TENA MJE MKIWA MMEVAA HIZI NGUO MLIZO ZIVAA NA KILA MMOJA WENU AJE NA MZAZI WAKE" KISHA MWALIMU AKAWAAMBIA WAWE HURU WAENDELEE NA MAMBO YAO ILA IKIFIKA SIKU YA IJUMAA TATU SIKU YA SHULE WAFANYE KAMA ALIVYO AGIZA MWALIMU HUYO PALE PALE JENIFER NA WENZAKE WAKAKOSA AMANI NA MUDI YA KUENDELEA KUFURAHI USIKU ULE IKATOWEKA NA KILA MMOJA WAO AKAWA ANAWAZA ITAKUAJE HIYO SIKU YA IJUMAA TATU NA WATAANZIA WAPI KUWAELEZA WAZAZI WAO JUU YA KOSA HILI WALILOFANYA MPAKA WAMEKUTANA NA MWALIMU KAWAOMBA WAENDE SHULE NA WAZAZI WAO.....?!
ITAENDELEA USIKOSE

MBINU ZA KUDUMU NA STAA KWENYE UHUSIANO!

UMEWAHI kujiuliza; kwanini mastaa wengi hawadumu na wenzi wao? Nimeamua kuchambua mada hii kwa sababu tunao mastaa wengi kwenye jamii yetu ambao wana uhusiano ama na mastaa wenzao au watu wa kawaida.

Pia, wapo watu ambao wanatarajia kuwa na uhusiano na mastaa, wakati kuna ambao tayari wapo ndani ya penzi na watu maarufu. Pamoja na hayo yote, wengi huwa wanashindwa kudumu kwa muda mrefu na mastaa kwa sababu za hapa na pale.
Katika mada hii ambayo nimeifanyia utafiti wa muda mrefu, itakufanya mpya katika uamuzi wako, ndani ya uhusiano na staa au staa ambaye yupo katika uhusiano na mwenzi asiye staa.
Labda tuwekane sawa kidogo, hapa namzungumzia mtu maarufu katika jamii, maarufu kwa maana ya kujulikana sana. Ustaa wa mtu unaweza kusababishwa na kazi au sanaa. Mathalani, sanaa za maigizo, soka, ndondi, riadha, siasa, urembo, utangazaji, uandishi wa habari, mitindo, utunzi, uchoraji, uchongaji, biashara nk.
Siwezi kutaja moja kwa moja majina ya mastaa, lakini naamini nimeeleweka vyema kuwa nawazungumzia watu wa aina gani. Watu wanaojulikana sana katika jamii kulingana na kazi zao za kila siku.
WASIKIE MASTAA
Wakati naandaa mada hii, nilipata bahati ya kuzungumza na baadhi ya mastaa ambapo walitoa maoni yao. Kwa bahati mbaya sana, wote niliopata kuzungumza nao, walipojua mazungumzo yetu yangeishia kuwa mada gazetini waliomba kuhifadhiwa majina yao.
Hebu wasikilize: “Kiukweli kaka Shaluwa, naweza kusema sisi wanawake wenyewe ndiyo wenye matatizo...asikudanganye mtu, ustaa kazi. Ukishakuwa maarufu, unataka mambo mengi; vipodozi, gari, nguo mpya, kujirusha, simu iwe na full vocha nk.
“Sasa kama unakuwa na boy ambaye anajifanya anakuchunga sana, inakuwa ngumu kudumu na sisi tulivyo jeuri, akikuacha asubuhi, jioni kiwanja unakutana na mwingine.”
Huyu ni staa wa muziki wa dansi nchini kama alivyozungumza nami jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
“Kiukweli huwa tunaacha sana mademu, lakini siyo suala la umalaya hapo brother Shaluwa. Kuna mambo mawili makubwa; kwanza, mwanamke anakuwa anapenda ustaa wako na siyo penzi la dhati, pili anakubana na kukupangia sana ratiba...niseme kwamba, wivu unazidi!
“Unajua unapokuwa msanii, unakuwa na mambo mengi, shoo kibao kila week-end, safari za mikoani nazo hazina idadi, club ndio usiseme, sasa kwa hali hiyo, lazima uwe na mwanamke smart kwa kila kitu.
“Tuongee ukweli, hakuna mtu anayekubali kuwa na mpenzi tapeli, sisi hatuna matatizo, lakini kama umefuata jina langu au pesa, nitakushtukia soon na hapo ndipo nitakapompiga kibuti na maisha yanaendelea,” ndivyo mmoja wa kinara katika Bongo Fleva anavyosema.
Hebu sikia kauli ya msanii huyu wa filamu: “Wanawake wanapenda umaarufu wetu, kwahiyo ukiwa naye siku mbili, ukimshtukia unamtema, hapo ndipo penye tatizo bro. Mimi sihitaji mtu anayependa jina langu, nahitaji penzi la dhati.”
TATIZO NI NINI?
Kikubwa ni katika KUELEWA na kutofautisha mapenzi na ustaa. Kama umempenda, umpende kwa mapenzi ya dhati, achana na ustaa wake, lakini lazima umjue mwenzi wako na uende naye jinsi anavyotaka.
Mapenzi ya kitapeli au kufuata mali na umaarufu hayana nafasi kabisa katika maisha ya sasa, yote yanawezekana lakini kwa kukubali kujifunza na kubadilika kulingana na mwenzi wako alivyo.
UPO KWENYE UHUSIANO NA STAA?
Kama nilivyotangulia kusema awali, sina maana kwamba mastaa wote hawawezi kuishi na wenzi wao bila kuwepo kwa migogoro, ni baadhi yao! Pamoja na kuwa na migogoro hiyo ambayo mwisho wake mara nyingi imekuwa ni kuachana, hakumaanishi kwamba, mastaa hawafai kuwa na wapenzi.
Hapa nataka kuzungumza na wale ambao tayari wapo katika uhusiano na mastaa na wale ambao wanatarajia kuwa na wenzi wenye majina makubwa kwenye jamii. Hebu pitia vipengele vifuatavyo;
Usiwe na wivu sana!
Ni kweli kwamba, kati ya alama za mapenzi ya dhati ni pamoja na wivu, lakini unapokuwa na uhusiano na mwenzi staa, lazima upunguze wivu. Hii haina maana kwamba, umuache awe kicheche, awe na mapatna wengi, hapana!
Mara nyingi mastaa huwa wanaiga mambo ya Kizungu, mathalani husalimiana kwa kukumbatiana, kuandikiana sms kwa maneno ya mapenzi kama dear, sweetie, mpenzi n.k, ukikutana na mazingira kama hayo, kuwa mpole, lakini fanya uchunguzi wako taratibu bila ya yeye kujua. Penye ukweli, uongo hujitenga.

Chapisha Maoni

0 Maoni